Home BIASHARA Mnada wa madini ya vito warejeshwa, kufanyika Desemba 14

Mnada wa madini ya vito warejeshwa, kufanyika Desemba 14

0 comments 516 views

Mnada wa madini ya vito ambao ulisimama kwa muda umepangwa kufanyika tena Desemba 14, 2024.

Waziri wa Madini Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mnada huo unaotarajiwa kufanyika katika mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, ili kuyaongezea thamani madini hayo.

Akizungumza Desemba 12, 2024, Mavunde amesema madini ya vito, yanafanyiwa mnada kama mkakati wa kuyatangaza na kuyaongezea thamani kimataifa.

Waziri Mavunde amesema utaratibu wa kufanya mnada huo ni jitihada za Serikali za kudhibiti utoroshwaji wa madini hayo nje ya nchi na pia kuwasaidia wachimbaji kuuza madini yao kwa bei ya ushindani inayoendana na soko la dunia.

Amesema, mnada huo utashirikisha wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi na atakayenunua madini hayo katika mnada ni atakayeshinda bei iliyowekwa.

“Mnada huu utaendeshwa kwa usalama mkubwa kwa kuwa madini hayo hususan Tanzanite yana thamani kubwa. Serikali imeimarisha ulinzi ili kujihadhari na watu wasio waaminifu,”amesema Waziri Mavunde.

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited