Home BENKI CRDB yapata kibali Hatifungani ya Kijani

CRDB yapata kibali Hatifungani ya Kijani

0 comments 383 views

Benki ya CRDB imekabidhiwa kibali cha kuuza Hatifungani ya Kijani “Kijani Bondi” ya miaka 5 yenye thamani ya dola za marekani Milioni 300 sawa na Sh. Bilioni 780 na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).

Kibali hicho cha kutoa hatifungani ya kijani kimekabidhiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa CMSA, Nicodemus Mkama kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyeambatana na Mwenyekiti wa Bodi, Dkt. Ally Laay katika hafla iliyofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam Agosti 24, 2023.

Kibali hicho kinaifanya Benki ya CRDB kuwa ya kwanza nchini kutoa hatifungani ya kijani, na ya kwanza kwa ukubwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Taarifa ya CRDB inasema Kijani Bond itarahisisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kufadhili miradi rafiki kwa mazingira na kuchochea ufikiaji wa Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDG).

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited