Home KILIMOKILIMO BIASHARA Serikali kujishughulisha na kilimo cha muda mfupi kudhibiti dola

Serikali kujishughulisha na kilimo cha muda mfupi kudhibiti dola

0 comments 631 views

Katika jitihada za kudhibiti dola Serikali ya Tanzania imesema inajishughulisha na kilimo hasa cha muda mfupi ambacho kinazalisha mazao kwa haraka.

Rais Samia Suluhu Hassan ameeleza hayo wakati wa hafla ya utoaji Tuzo za Rais kwa wazalishaji bora (President’s Manufacturer of the year Awards – PMAYA) katika ukumbi wa Super Dome, Masaki.

Ameeleza kuwa mbali na kukua kwa sekta ya utalii nchini, Serikali pia imedhamiria kujishughulisha na kilimo cha muda mfupi ili kuthibiti dola nchini.

Katika hafla hiyo, Rais Samia amewataka wazalishaji wa bidhaa kupitia Shirikisho la wenye Viwanda Nchini (CTI) kuendelea kuimarisha ubora wa bidhaa wanazozalisha.

Amesema serikali imeimarisha miundombinu ya barabara ba bandari ili bidhaa zinazozalishwa zisafirishwe nhje na kuingia nchini ili sekta ya viwanda iendelee kufanya vizuri.

Rais Samia amewataka wazalishaji kuongeza juhudi katika uzalishaji na uongezaji wa bidhaa (intermediate goods) ili kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi.

“Serikali inatarajia kuwasha kinu cha kwanza cha kufua umeme mwezi Januari 2024 katika bwawa kwa Nyerereikiwa ni jitihada za kuzalisha umeme wa kutosha ambao ni muhimu kwa wazalishaji,” ameeleza Rais Samia.

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited