Home BIASHARAUWEKEZAJI Rais Samia akaribisha wawekezaji wa India

Rais Samia akaribisha wawekezaji wa India

0 comments 492 views

Rais Samia Suluhu Hassan amewakaribisha wawekezaji wa India kuja kuwekeza Tanzania akiahidi mazingira rafiki ya biashara na maendeleo ya uchumi.

Mkuu huyo wa nchi, ameyasema hayo New Delhi wakati akizungumza na wawekezaji katika jukwaa la biashara na uwekezaji la Tanzania-India katika ziara yake ya siku tatu nchini India.

Rais Samia amesema Tanzania inatekeleza maendeleo na mageuzi ya uchumi ya Afrika yanayochochewa na sekta binafsi na uwekezaji katika kukuza uchumi.

“Kama sehemu ya mageuzi hayo, Tanzania tunatumia teknolojia ambayo inawawezesha wawekezaji kutoka nje ya nchi kuweza kusajili biashara zao kwa njia ya mtandao kabla ya kufika nchini,” ameeleza Rais Samia.

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited