Home Elimu Afrika Mashariki yatakiwa kuendeleza Kiswahili

Afrika Mashariki yatakiwa kuendeleza Kiswahili

0 comments 340 views

Wito umetolewa kwa nchi za Afrika Mashariki kuendeleza matumizi ya kiswahili katika maeneo muhimu ya kiutawala na kijamii.
Rais mstaafu wa Msumbiji Joaquim Chissano ametoa wito huo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utoaji Tuzo ya Taifa ya Mwl. Nyerere ya Uandishi Bunifu.

Ameeleza kuwa kiswahili ni tunu na utambulisho wa afrika na mwafrika.

Akiongelea kuhusu tuzo hizo Chissano amesema Juhudi za kutambua mchango wa wadau wa maandiko bunifu kwa lugha ya kiswahili ni muhimu na kwamba juhudi hizi ziendelezwe kwani uhai wa lugha yoyote duniani ni kuwapo na machapisho yaliyoandikwa kwa lugha hiyo.

“Ni wazi Mwl. Nyerere kwa dhati kabisa aliikuza lugha ya kiswahili kwa kuandika maandiko bunifu kama riwaya, mashairi na kutafsiri kazi mbalimbali za fasihi ya kingereza katika kiswahili hivyo ni heshima kubwa tuzo hii kupewa jina lake,”amesema Rais Chissano.

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited