Home Elimu Tanzania kuendelea kuboresha miundombinu ya elimu

Tanzania kuendelea kuboresha miundombinu ya elimu

0 comments 408 views

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Zainabu Katimba amsema serikali inatambua umuhimu na itaendelea kuboresha miundombinu ya Elimu ikiwemo Mabweni ya wanafunzi, uzio, majengo ya utawala na mabwalo kupitia miradi mbalimbali.

Katimba amesema hayo Bungeni Jijini Dodoma katika kipindi cha Maswali na Majibu, wakati akijibu Swali la Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini Reuben Kwagilwa aliyetaka kujua, je ni lini Serikali itajenga bwalo la chakula, majengo ya utawala na mabweni ya wanafunzi katika Shule ya Sekondari Misima na Handeni?

“Kwa kutambua umhimu mkubwa sana wa miundombini hii katika shule zetu, Serikali itaendelea kutenga fedha kwenye bajeti kwaajili ya kuendelea kujenga miundombinu ya bwalo, majengo ya utawala, mabweni ya wanafunzi na uzio.

Hii ni katika Shule za Sekondari kote nchini zikiwemo Shule za Sekondari Misima na Handeni kupitia miradi mbalimbali ya elimu,” ameeleza Katimba.

Aidha, Katimba amesema Serikali inajenga shule 26 za bweni za wasichana za kitaifa katika Mikoa yote nchini kupitia mradi wa Sequip kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza zilijengwa katika Mikoa kumi na awamu ya pili zitajengwa katika Mikoa kumi na sita huku zikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 4.1.

Katimba amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Innocent Edward Kalogeris aliyehoji ni lini Serikali itajenga shule maalumu ya Sekondari ya wasichana Dutumi katika Kata ya Bwakila, Morogoro vijijini.

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited