Home BIASHARAUWEKEZAJI Sekta binafsi changamkieni fursa: Rais Samia

Sekta binafsi changamkieni fursa: Rais Samia

0 comments 367 views

Rais Samia Suluhu Hassan imeitaka Sekta Binafsi nchini kuchangamkia fursa ya kujenga hoteli kwa ajili ya watalii.

Rais Samia amesema hayo wakati akifungua na kushiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) Ikulu, jijini Dar es Salaam.

“Wageni wanaokuja mwakani na mwaka unaofuata watakosa mahali pa kulala kama hatukuchangamka kwenye kujenga hoteli sasa hivi, sekta binafsi ni fursa muhimu” amesema Rais.

Amesema tafiti ndogo iliyofanyika inaonyesha kuwa wageni waliokuja mwaka jana ni asilimia 30 tuu wamerudi mwaka huu.

Amesema hii inaonesha kuwa Tanzania wageni wanakuja lakini hawataki kurudi pamoja na vivutio vilivyopo.

Ameitaka sekta ya utalii kuangalia kasoro zilizopo na kuzifanyia marekebisho ili wageni wawe wanarudi na kuwafanya wenzao kuja Tanzania.

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited