Serikali yataka ubunifu wa Watanzania ulindwe
Serikali kupitia Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara imetaka ubunifu wa Watanzania ulindwe na kuendelezwa. Naibu Waziri wa Wizara hiyo Exaud Silaoneka Kigahe amesema vijana wengi Watanzania wana ubunifu lakini bunifu hizo huchukuliwa na watu wengine kutokana na kutolindwa kisheria. Ameeleza kupitia taasisi za Wizara ambazo ni Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania…
