Tanzania yaikaribisha kampuni za China kuwekeza Sekta ya Nishati
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian ambapo wamezungumza masuala mbalimbali ikiwemo uhusiano uliopo kati ya Tanzania na China na uwekezaji kwenye miradi ya Nishati. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam Novemba 24, 2023 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali…
