Serikali kutoa mafunzo ya kilimo biashara kwa vijana
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imetangaza fursa ya mafunzo ya kilimo biashara kwa vijana. Mafunzo hayo ambayo ni awamu ya kwanza yanatarajiwa kufanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Kilimo Bihawana mkoani Dodoma kuanzia Februari 15, 2023. Katika mafunzo hayo wanufaika ambao ni vijana watapatiwa elimu ya kilimo biashara kwa muda wa miezi mitatu ambapo baada…
