wew

Benki zatakiwa kupunguza riba

Benki mbalimbali nchini zimetakiwa kupunguza riba, ili kutoa fursa kwa wateja kukopa na kufanya uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali. Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Felician Mtahengerwa ametoa rai hiyo jijini Arusha katika mkutano wa wadau wa Benki ya Maendeleo (TIB), Kanda ya Arusha. Mtahengerwa amesisitiza kuwa endapo benki zikipunguza riba katika mikopo, Watanzania wengi wataweza kukopa…

Soma Zaidi
WhatsApp Image 2023 06 19 at 15.21.41

Wakulima wapewa mafunzo sumukuvu

Wakulima wilayani Kiteto mkoa wa Manyara wamepewa mafunzo juu ya Sumukuvu na madhara yake. Mafunzo hayo, yametolewa na Wizara ya Kilimo kupitia Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu Tanzania (TANIPAC). Elimu hiyo imetolewa kwa wahanga wa madhara ya sumukuvu ambapo imelenga uvunaji, ukaushaji na uhifadhi wa nafaka kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo ili kuepusha chakula kisichafuliwe…

Soma Zaidi
WhatsApp Image 2023 06 13 at 17.29.32

Serikali kusajili wakulima

Katika kuboresha kilimo nchini, serikali imesema itafanya usajili wa wakulima ili kujua idadi gani ya watu wanajishughulisha kwenye kilimo. Rais Samia Suluhu Hassan amesema hayo wakati akihutubia katika tamasha la utamaduni lililofanyika Bulabo mkoani Mwanza. “Tunakwenda kuweka jitihada mbalimbali ili tukuze kilimo chetu. Cha kwanza tunachokifanya na ninaomba wakulima mnisikilize vizuri ni usajili wa wakulima…

Soma Zaidi
WhatsApp Image 2023 06 13 at 15.09.58

Tanzania kusaini mkataba ukaguzi miamala ya kimataifa

Serikali inatarajia kusaini mkataba ambao utaiwezesha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kupata taarifa mbalimbali kutoka nchi 146 duniani ambazo zitasaidia katika kuongeza ufanisi wa ukaguzi wa miamala ya kimataifa. Hayo yamebainishwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Hamad Hassan Chande, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, aliyetaka kujua…

Soma Zaidi
WhatsApp Image 2023 06 13 at 10.28.58

Vijana wenye biashara changa kunolewa

Biashara changa za vijana 196 (startups) zimeingia katika hatua ya mafunzo kabla ya kupewa mitaji wezeshi kwa ajili ya kuendeleza biashara zao. Taasisi ya CRDB Bank Foundation imezindua kambi ya mafunzo (boot camp) kwa ajili ya vijana hao. Uzinduzi wa kambi hiyo umefanyika katika kituo maalum cha kuendeleza biashara changa kilichopo Makao Makuu ya zamani…

Soma Zaidi
WhatsApp Image 2023 06 13 at 10.29.25

Wanawake kupata mafunzo na mitaji wezeshi

Benki ya CRDB imesaini makubaliano ya kushirikiana na taasisi za BUTA Vicoba Endelevu na Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) kuwawezesha wanawake kupata mafunzo na mitaji wezeshi kupitia program ya IMBEJU. Akizungumza kwenye hafla ya makubaliano hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa amezishukuru taasisi hizo kwa utayari wao wa kushirikiana na…

Soma Zaidi
Enable Notifications OK No thanks