Kibegi, jezi za Simba zilizopandishwa Ml. Kilimanjaro zaleta Sh 29m

WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.02

Klabu ya Simba imefanya mnada wa kibegi na jezi zilizopandishwa Mlima Kilimanjaro kwa Sh29 milioni.

Jezi hizo za msimu wa mashindano 2023/24, zilizinduliwa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro Julai 21, 2023.

Jezi hizo za aina tatu ambazo zimepigwa mnada ni zenye majina ya viongozi, Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Ali Mwinyi.

Pia, kuna ya Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson.

Taarifa ya klabu ya Simba inaeleza kuwa katika mnada huo jezi ya Rais Dk. Samia imeuzwa kwa Sh. 10,000,000 huku ile ya Rais Dk Mwinyi imeuzwa kwa Sh 5,000,000.

WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.03 3

Jezi ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa imenunuliwa kwa Sh. 4,000,000 na ya Makamu wa Rais Dk. Mpango imeuzwa Sh. milioni 3.

WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.03 1WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.03 2

Katika manada huo, milioni 2,500,000 zilitolewa kununua jezi ya Spika wa Bunge Dk. Tulia huku jezi ya Rais wa Heshima wa klabu, Mohamed Dewji ikinunuliwa kwa Sh. 2,000,000.

WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.03 5WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.03 4

“Kibegi kilichokuwa na jezi zetu na kupelekwa juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro kimeuzwa kwa Sh. 2,500,000,” imesema taarifa hiyo.

WhatsApp Image 2023 08 01 at 14.13.03

Fedha zilizopatikana katika mnada huo zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa wodi ya mama na watoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali ya Taifa ya Zanzibar (Mnazi Mmoja).


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks