Mgodi mkubwa wa dhahabu kuanzishwa Hanang’, Manyara
Waziri wa Madini Anthony Mavunde amefanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Marvel Gold Timothy Strong juu ya uwekezaji wa kampuni hiyo kwenye sekta ya madini. Kampuni hiyo kutoka nchini Australia imefika kujitambulisha Aprili 09, 2025 na kuelezea mpango wao wa kuanzisha mgodi mkubwa wa dhahabu katika Wilaya ya Hanang’ Mkoa wa Manyara….
