Tanzania yaja na mpango kuwawezesha waraibu wa dawa za kulevya kiuchumi
Serikali ya Tanzania inaanda mpango wa Kitaifa wa kuwawezesha kujikimu kiuchumi vijana wanaoachana na matumizi ya dawa za kulevya. Mpango huo, utawawezesha vijana hao kupata mitaji ambayo itawawezesha kushiriki kwenye shughuli za ujasiriamali ambazo zitawasaidia kukuza kipato chao. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameeleza hayo Juni 30, 2024 wakati akizungumza na wananchi na wadau mbalimbali walioshiriki…
