Taasisi 50 kushiriki kongamano la biashara

Usione aibu kufanya biashara ya halali inayokuingizia kipato umaskini ni aibu kubwa zaidi. 34

Takribani Taasisi 50 zinatarajiwa kushiriki Kongamano la Biashara la Kimataifa  lililoandaliwa na Jukwaa lijulikanalo kama ‘China Trade Week’ (CTW) na kuwahusisha wafanyabiashara mbalimbali wa ndani na nje ya nchi.

Kongamano hilo litakalohusisha maonesho zaidi ya bidhaa 200, litafanyika  Septemba 26 hadi 28 katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.

Bidhaa hizo ni pamoja na bidhaa za kielektroniki, afya, viwanda, mavazi, urembo na ujenzi.

Kwa mujibu wa waandaaji wa kongamano hilo, Zahor Ahmed, amesema tukio hilo linalofanyika kwa mara ya kwanza nchini pamoja na mambo mengine limelenga kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na China.

“Kongamano hili limelenga kufungua  uchumi wa kimataifa kwa mataifa haya mawili na dunia nzima, biashara itakuwa mstari wa mbele kuleta maendeleo taifa,” ameeleza Ahmed.

Amebainisha kuwa kongamano  hilo ambalo Tanzania itakuwa taifa la sita kuwa mwenyeji limeshafanyika katika nchi za Kenya, Ethiopia, Afrika Kusini, Ghana na Morocco yakijumuisha maonesho ya bidhaa mbalimbali.

Mbali na faida  za  kiuchumi, kongamano hilo pia litasaidia uwekezaji na kubadilishana tamaduni zilizohusu sekta za ujenzi wa miundombinu, nishati, kilimo, chakula, sayansi na teknolojia.


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks