Rais Samia aahidi kufanya “Royal Tour” kuitangaza hifadhi ya Katavi

WhatsApp Image 2024 07 17 at 12.35.28

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kufanya filamu nyingine ya Royal Tour katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi baada ya kujionea wanyamapori mbalimbali katika Hifadhi hiyo.

Dkt. Samia ameyasema hayo Julai 15, 2024 wakati akizungumza na wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, Mkoani Katavi.

Kauli hiyo inafuatia ombi la Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda, la kuomba Royal Tour nyingine ifanyike mkoani humo.

WhatsApp Image 2024 07 17 at 12.34.55
Hifadhi ya Katavi

“Nataka nikiri kwamba zile sifa alizozisema Waziri Mkuu Mstaafu kuhusu uwepo wa wanyama wengi na wa kuvutia katika Hifadhi ya Katavi nimeziona mwenyewe na zimetimia maana leo nilipita kwenye mbuga hiyo kuona ikoje mahitaji yakoje” amesema Rais Samia na kusisitiza:

“Tumeona mambo mengi ya kufanya mle ndani na suala la Royal Tour Waziri wa Maliasili na Utalii ameshaandika hivyo jipange na ukiwa tayari mimi mwenyewe nitakuja.

WhatsApp Image 2024 07 17 at 12.35.17

Soma: Royal Tour yaongeza mapato kutoka Tsh 70bn hadi Tsh 84bn


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks