Waziri ataja sababu daraja la Tanzanite kutumika bure

WhatsApp Image 2022 02 04 at 2.36.32 PM

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema daraja la Tanzanite Watanzania hawalipi na hawatalipa kwa sababu limejengwa kwa 100% kwa pesa ya serikali.

Waziri Mbarawa amebainisha kuwa fedha hizo ni mkopo wa masharti nafuu kutoka Korea Kusini ambazo zitalipwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia zote.

“Daraja la Kigamboni utaratibu uliotumika ni tofauti, pale serikali iliingia makubaliano na NSSF kwa ajili ya uwekezaji ule.

Na baada ya NSSF kuwekeza ile pesa lazima irudi. Na ndio tukakubaliana kwamba pale daraja lile watu watalipa tozo ndogo ili waweze kuchangia katika kurejesha pesa iliyotumika na NSSF” amesema Waziri.

Ameeleza kuwa huo ndio utaratibu na utaratibu huu unatumika maeneo mengi duniani sio hapa Tanzania tuu.

Daraja la Tanzanite(Salenda) lilianza kutumika rasmi February Mosi, 2022.

Soma: Ujenzi daraja la Tanzanite wakamilika


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks