Wanahabari za michezo kunolewa kwa ajili ya AFCON

WhatsApp Image 2024 02 12 at 14.05.28

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye amesema Serikali kupitia Wizara anayoiongoza na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, itawezesha mafunzo ya ndani na nje ya nchi kwa waandishi wa habari za michezo kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027.

Akifungua TASWA Media Day Bonanza kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa katika viwanja vya Msasani Beach Club, Dar es Salaam, Februari 10, 2024, Waziri Nape amesema, “Serikali kupitia Wizara ya Habari na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo tutandaa mafunzo pamoja na safari za nje ya nchi kwa waandishi wa habari za michezo ili kujiandaa vizuri katika kutoa habari za mashindano ya AFCON 2027.

Wanahabari ni watu muhimu katika kutangaza nchi yetu. Tunapenda kuwapa mafunzo na vifaa ili waweze kutangaza mashindano hayo kwa ufanisi.”

Aidha, Waziri Nape amewataka wanahabari kuepuka kuandika habari zinazowavunja moyo wa wanamichezo wa Tanzania, akisisitiza kuwa michezo ni mchanganyiko wa mafanikio na changamoto, hivyo ni muhimu kutoa msaada na uungwaji mkono kwa wanamichezo wetu.

“Tusiandike habari zinazowavunja moyo wanamichezo wetu,” amesisitiza.


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks