Vijana wanasajili bunifu nchi jirani: Nape

WhatsApp Image 2023 11 01 at 16.54.19

Kukosekana kwa Sera ya kampuni changa (Startups) kunawafanya baadhi ya vijana wa Tanzania kusajili bunifu zao nchi jirani.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema hayo katika kikao cha wadau mbalimabli kutoka ndani na nje ya nchi cha kujadili ushirikiano wa maendeleo juu ya uundwaji wa Sera ya Kampuni Changa za TEHAMA (Startups) Tanzania kilichofanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba jijini Dar es Salaam.

Waziri Nape amesema kuwa baadhi ya vijana wabunifu wa TEHAMA imewabidi wakasajili bunifu zao katika nchi za jirani kutokana na kutokuwepo kwa Sera ya Startups nchini.

“Bahati mbaya kwa muda kidogo nchi yetu imekuwa haina mfumo mzuri wa kisheria wa vijana hawa wanaofanya ubunifu katika TEHAMA na mara nyingi wamelazimika kwenda nje ya nchi ili kusajili bunifu zao.

Kama Serikali tukasema inabidi tuwe na mfumo mzuri utakaotambua bunifu za hawa vijana lakini pia uweze kuzilinda bunifu hizo ili pia waweze kuvutia uwekezaji nchini,” amesema Waziri Nape.

Amebainisha kuwa serikali imekubaliana na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, kuweka misingi na wako tayari kuendelea na hatua inayofuata ili kukamilisha sera hiyo mapema.

Kikao hicho pia kimewahusisha Wadau mbalimbali wakiwemo Wadau wa Maendeleo nchini, Chama cha Tanzania Startups Association, Taasisi za Serikali na Wizara mbalimbali.

WhatsApp Image 2023 11 01 at 16.54.28


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks