Wawekezaji waitwa Iringa kuwekeza sekta ya madini
Wito umetolewa kwa wawekezaji wote nchini kuchangamkia fursa za uwekezaji zilizopo katika Sekta ya Madini mkoani Iringa ambapo mkoa huo umebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali ikiwemo dhahabu, vito, chuma, madini ya viwandani na madini ya ujenzi. Wito huo umetolewa na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhandisi AbdulRahman Milandu wakati akizungumza katika…
