Benkiwakala inaleta ushindani huduma za bima: Mwigulu

ppp

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amesema Mfumo wa Benkiwakala wa Bima umesaidia kukuza biashara ya Bima nchini.
Dk Mwigulu ameeleza hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Morogoro Kusini Innocent Edward Kalogeris aliyetaka kujua kama Serikali haioni kuwa kuruhusu Benki kuwa Wakala wa Bima, Mawakala wengine watafunga biashara kwa kukosa wateja.
Dk. Nchemba amesema Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na wadau wa bima ilianzisha Benkiwakala wa Bima ili kuongeza wigo wa usambazaji na upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi.

“Idadi ya Wakala wa Bima wa Kawaida imekuwa ikiongezeka sambamba na Benkiwakala wa Bima kwa sababu hali hii imechochea ushindani, ubunifu na kutegemeana”, amebainisha Dk. Nchemba.

Amesema Takwimu zinaonesha Benkiwakala waliosajiliwa ni 14 kwa mwaka (2020), 23 (2021), 27 (2022) na 30 hadi Machi 2023.

Kwa upande wa Wakala wa Bima wa kawaida waliosajiliwa ni 745 kwa mwaka (2020), 789 (2021), 910 (2022) na 960 kati ya Julai 2022 na Machi 2023.


Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks