Watanzania watakiwa kumuenzi Lowassa kwa uzalendo na uwajibikaji

WhatsApp Image 2024 02 13 at 14.41.28

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema namna bora ya kumuenzi Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Ngoyai Lowassa ni kuendelea kuyaishi maono yake ya uzalendo, uwajibikaji ili iwe dira ya kuzidi kujenga umoja na kupiga hatua za maendeleo nchini.

Rais Dk. Mwinyi amesema hayo wakati akitoa salamu za pole na kutoa heshima za mwisho kwa Hayati Lowassa katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam Februari 13, 2024.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ametoa salamu za Pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan, familia na wananchi wote kwa msiba huu.

Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi ameeleza kuwa amejifunza mengi kutoka kwa Hayati Lowassa ukiwemo uzalendo, uwajibikaji, ushirikiano na watu wa makundi yote na kuweka mbele maslahi ya nchi.

Hayati Lowassa alifariki Februari 10, 2024 na anataraji kuzikwa Februari 17, 2024 Wilayani Monduli.

WhatsApp Image 2024 02 13 at 14.41.23
Rais Hussein Mwinyi na Mkewe Mariam Mwingi wakitoa heshima za mwisho kwa Hayati Edward Ngoyai Lowassa.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Discover more from PesaTu – Habari za Biashara na Uchumi Tanzania

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Enable Notifications OK No thanks