Home Elimu WALIOPONA CORONA TANZANIA WAFIKIA WATANO

WALIOPONA CORONA TANZANIA WAFIKIA WATANO

0 comments 391 views

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ametangaza kupona kwa wagonjwa wawili zaidi wa virusi vya Corona na hivyo kufanya idadi ya waliopona ugonjwa huo kufikia watano.

Wagonjwa waliopona ni kutoka Dar es Salaam na Arusha. “Takwimu za leo kutoka maabara kwa waliochukuliwa sampuli hakuna maambukizi, wenye corona Tanzania wanabakia 24, Zanzibar 7 na Bara 17, leo tumepata wagonjwa wawili ambao wamepona, wa DSM na Arusha(jumla TZ wamepona watano), kwahiyo sasa hatuna mgonjwa corona Arusha na Kagera”-Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Pesatu ni jukwaa la habari, elimu ya kifedha, na ujasiriamali Tanzania. Tunakuletea taarifa mpya za biashara, uwekezaji, ajira, kilimo, mitindo, na burudani, pamoja na mwongozo wa kufanikisha mafanikio yako. Kwa makala zetu, mwongozo wa vitendo, na taarifa za hivi punde, tunasaidia wajasiriamali, vijana, na jamii kupata maarifa yanayoweza kubadilisha maisha yao na kuongeza fursa za kifedha.

Jarida la Habari

PESATU – Haki Zote Zimehifadhiwa. Imetengenezwa na Mediapix Limited